×

Waziri Makamba Afunguka Mikakati Ya Kuboresha Mazingira

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Yusuph Makamba akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Global Publishers, leo Jumatano.
Meneja wa Global Publishers (mwenye tai) akizungumza na Waziri January Makamba.
Waziri Makamba akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Global.
Wafanyakazi wa Global wakiendelea kumsikiliza kwa makini Waziri Makamba (hayupo pichani).
Waziri Makamba alipokuwa akiwasili Global.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano na Mazingira, January Yusuph Makamba, leo Jumatano alitembelea ofisi za Global Publishers na kupata nafasi ya kuwasalimia wafanyakazi. Katika mazungumzo yake mafupi ofisini hapo, waziri alisisitiza uwepo wa mikakati mizuri ya kuendelea kuboresha mazingira na kuudumisha muungano.

Aidha Waziri Makamba amewasisitiza Watanzania kuendelea kuiunga mkono serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika kuboresha mazigira ili kuifanya Tanzania iendelee kuwa nchi yenye amani na mazingira bora.

Leave a Comment