





MSANII zao la Bongo Star Search (BSS) Kayumba Juma jana alikuwa kivutio kikubwa wakati wa tamasha la Mziki Mnene linaloendeshwa na kituo cha redio cha Efm na Tv E, uliofanyika katika ukumbi wa Msasani Klabu Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Sambamba na Kayumba, msanii mkongwe rapa Chid Benz, na kundi la akina dada sita kutoka kundi la Mkubwa Fella nao walitoa burudani kali huku burudani ya muziki ikitoka kwa RDJ’s.
Awali, wakati wa mchana, katika viwanja vya Biafra Kinondoni, kulikuwa na zoezi la kusaka vipaji vya muziki wa Singeli Michano ambapo mshindi wa kila wilaya watapata nafasi ya kurekodi bure.
Wiki ijayo itakuwa zamu ya wilaya ya Ubungo hivyo wasikilizaji wa 93.7 EFM watapata burudani ya aina yake kutoka kwa timu nzima ya EFM redio.