MBUNGE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mohammed Razar, amemkabidhi msaada wa chakula kwa Waziri, Kassim Majaliwa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wenye uhaba wa chakula.
Mbali na hilo, Razar amempa nafasi Majaliwa amchagulie mikoa mitano ambayo itafanyiwa mashindano na kila mkoa utatoa timu ya taifa ya michezo ya watoto wa shule, ambapo mashindano hayo atayagharamia yeye mwenyewe kuanzia jezi, mazoezi na vitu vingine.
Aidha, Razar ameelezea dhamira yake ya kutaka mashindano hayo yaanzishwe ni kutokana na timu za mpira Tanzania, kuwa na idadi kubwa ya wachezaji kutoka nchi jirani kuliko wale wanaotoka nyumbani, hivyo anachokitaka ni kuzalisha vipaji na kuvikuza vije kuchezea timbu zao hapo baadae.