
MAJONZI, VILIO na simanzi vimetawala wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini aliyeuawa kwa kupigwa risasi Feb 16, 2018.

Baada ya mwili wa marehemu kuwasili katika viwanja vya NIT kwa ajili ya kuagwa, wanafunziwa chuo hicho walianza kulia kwa majonzi na uchungu huku wengi wao wakioanguka na kupoteza fahamu kutokana na kuguswa na msiba huo uliotikisa taifa zima la Tanzania.

Mwili wa Akwilina umeagwa leo katika viwanja vya Chuo cha NIT na kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Rombo Mashati kwa mazishi.


Global Publishers na Global TV Online inatoa pole kwa ndugu, marafiki, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba wa Akwilina.

Mwenyezi Mungu ailaze mahali pema peponi roho yua marehemu. AMEN!






PICHA NA RICHARD BUKOS | GPL