×

Banda: Ukiwaambia Sauz Mimi Mtukutu, Watakushangaa

Mtanzania pekee mwenye uhakika wa namba katika Ligi Kuu Afrika Kusini Afrika Kusini, Abdi Banda.

 

MJI mdogo wa Polok­wane upo Kaskazini mwa jimbo maarufu zaidi nchini Afrika Kusini la Gauteng.

Makao makuu ya Gauteng ni upande wa jiji kubwa zaidi Afrika Kusini la Johannesburg. Kutoka ka­tika jiji hilo ni mwendo sa­hihi wa saa tatu kufika katika mji huo mdo­go.

 

K w a w a n a o ­f u a t i l i a michezo, P o l o k ­w a n e ni kati ya miji iliyokuwa wenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia ili­yofanyika kwa mara ya kwanza na mwisho hadi sasa barani Af­rika, hiyo m w a k a 2010.

 

Maana ya neno Polok­wane ni “eneo s a l a m a ” , huko ndiyo anaishi Mtan­zania, Abdi Banda, kijana aliyechipukia kisoka katika klabu ya Coastal Union ya Tanga.

 

Banda anaishi Afrika Kusini katika mji huo wa Polokwane ingawa maisha yake yame­kuwa ni kutembea kutoka mji mmoja kwenda mwingine na si rahisi kubaki Polokwane angalau kwa wiki mbili mfu­lulizo kutokana na majukumu yake.

Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally Jembe (kulia) akiwa na beki wa Baroka FC, Abdi Banda, Mtanzania pekee mwenye uhakika wa namba katika Ligi Kuu Afrika Kusini Afrika Kusini.

Polokwane timu maarufu zaidi ni Polokwane City ambayo hata hivyo kipindi hiki imekuwa iki­poteza umaarufu kutokana na mwendo mzuri ilionao Baroka FC katika Ligi Kuu ya Afrika Kusi­ni pamoja na michuano mingine ya makombe mbalimbali.

 

Mwendo mzuri wa Baroka FC unaifanya timu hiyo kuzidi kuji­zolea mashabiki na kupata sapoti kubwa kutoka kwa watu wa eneo la Polokwane. Banda ni beki wa timu ya Baroka FC, ni beki tege­meo na sasa kivutio cha mashabi­ki wengi wanaomuona ni kama mchezaji staa na tegemeo namba moja katika kikosi hicho.

Umaarufu wa Banda umeku­wa ukikua kwa kasi kubwa na hii ina­tokana na kuaminika zaidi na benchi la ufundi na namna ambavyo ame­kuwa akiifanya kazi yake kwa ufa­saha mkubwa.

Championi kama ilivyo kawaida yake, limeamua kufunga safari hadi nchini Afrika Kusini kumshuhudia Banda akiwa kazini na kujifunza men­gi kuhusi­ana na kazi yake anayoi­fanya.

Wakati a k iondoka Tanzania na ku­jiunga na Baroka FC, ilionekana ni vigumu Banda ku­fika mbali, lakini sasa ni gumzo kuu na tegemeo katika kikosi hi­cho na tayari ameanza kuwa kivutio kwa baa­dhi ya timu kubwa za Afrika Kusini.

 

Katika mahoji­ano hayo ya moja kwa moja hapa Af­rika Kusini, Banda anazungumza mengi ambayo asilimia 99 hukuwahi kuyasikia.

 

Anaeleza safari yake ya Afrika Kusini, hatua alizopiga na chamgamoto. Tutak­wenda taratibu kwa hatua k u ­

jua mengi yakiwemo yale ambayo aliyapata kama changamoto wakati akiwa anacheza Tanzania na nini sasa anataka baada ya hatua nzuri aliyopiga na Baroka FC.

 

Banda anasema, kitu cha kwanza ambacho kilimsaidia kupiga hatua na kufika mbali ni malengo makubwa aliyoku­wa amejiweka kutaka kutoka nje ya Tanzania na kucheza nje.

CHAMPIONI: Malengo wengi wanaweka lakini wameshind­wa kuyatimiza, wewe ilikuwa­je ukafanikiwa?

 

BANDA: Kila mmoja huwa ana­panga kivyake lakini utekelezaji wa malengo ndiyo tatizo kubwa zaidi. Mimi nataka kufuyafikia malengo yangu.

 

CHAMPIONI: Wakati ukiondo­ka kuja Afrika Kusini haukupe­wa nafasi ya kufanya vizuri, un­afikiri Tanzania ulikosea wapi?

 

BANDA: Tanzania kuna mambo mengi sana ambayo yanamfan­ya mchezaji ashindwe kucheza. Naamini tutayazungumzia lakini vitu ni tofauti sana.

 

CHAMPIONI: Wewe ulisifika kwa utukutu na mara nyingi ulione­kana hausikilizi?

BANDA: Hapa Afrika Kusini ukiwaambia mimi ni mtukutu watashangaa sana, lakini ukweli mimi ni mpambanaji na mtu ninayetaka kushinda kwa kila ninachokifanya au kukutana.

 

CHAMPIO­NI: Umeweza vipi kue­ndana na utamaduni wa soka la Afrika Kusini kwa maana ya nidhamu ya juu, mambo kwa mpangilio wakati ulizoea Tanzania mam­bo ya kubabia?

 

BANDA: Kweli mambo ni kwa mipangilio, ratiba na utaratibu sahi­hi. Nimeona huu ni utama­duni na utaratibu sahihi ambao wanatumia, ni lazima niufuate na naona ni vizuri.

 

CHAMPIONI: Tanzania huku­fuata utaratibu, hapa uliweza vipi, ilikuwa ina shida kwako au ulichukua muda gani kue­ndana na wenzako?

 

BANDA: Kulikuwa na ugumu, lakini kwangu ilikuwa kidogo sana kwa kwa kweli. Baada ya muda nikaweza kuendana nao. Napenda kufuata utaratibu tokea nikiwa Tanzania. Lakini kama viongozi wako hawafuati utaratibu, wachezaji wenzako hali kadhalika, unafikiri wewe utafuataje utaratibu kwa asil­imia mia? Hapa watu wanafuata utaratibu na mimi naendana nao.

 

CHAMPIONI: Udhibiti wa sua­la la nidhamu ukoje hapa?

BANDA: Nidhamu ni jambo namba moja katika mpira wa Afrika Kusini. Hawa jamaa wako tayari kuku­ondoa katika kiko­si mara moja bila ya kuangalia sura kama utafanya utovu wa nidhamu, yaani hata kama wanakutegemea kwa asilimia elfu moja.

STORI NA SALEH ALLY | GLOBAL PUBLISHERS