×

YANGA WAIBIPU SIMBA SC

MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hussein Niyika amesema endapo timu hiyo itaibuka na ushindi dhidi ya Township Rollers ya Bot­swana, basi Simba ijiandae ku­kumbana na kipigo kikali kwe­nye mchezo wa Ligi Kuu Bara.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, Nyika alisema: “Tupo Botswana hivi sasa tukiendelea na mikakati yetu ya kuhakikisha tunawafunga Township Rollers lakini pia tunajiandaa na mechi yetu na Simba ambayo tutaku­tana nayo hivi karibuni.

 

“Hata hivyo, endapo tutashin­da mechi hiyo ya kesho basi Sim­ba wajiandae kwa kipigo kwani tutakuja kwa nguvu mpya katika mechi hiyo ya ligi kuu.

“Nasema hivyo kwa sababu vijana wetu wana ari lakini pia nguvu mpya ya kupambana to­fauti na awali.”

Sweetbert  Lukonge, Dar es Salaam.