×

Mama Jide Aagwa Dar, Kuzikwa Bunda – Mara

Jeneza lenye mwili wa marehemu Martha Mbibo.

 

MWILI wa mama mzazi wa msanii wa Bongo Fleva, Judith Mbibo Wambura ‘Lady Jaydee au Jide’, Bi. Martha Mbibo umefanyiwa ibada na kuagwa nyumbani kwake Kiwalani jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwenda Bunda mkoani Mara kwa maziko.

Bi. Martha alifariki dunia juzi nyumbani kwake kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya saratani kwa muda mrefu.

Mbunge wa zamani wa Bunda na waziri mstaafu wa kilimo na mifugo, Steven Masatu Wassira (aliyenyoosha mkono) akiwa na waombolezaji wengine msibani hapo.

Marehemu ameacha watoto wanane kati ya kumi ambapo wawili  walishatangulia mbele za haki.

Jide (katikati) akiwa na ndugu zake wakati wa ibada.

Katika familia hiyo, Jide ni mtoto wa tisa miongoni mwa hao kumi.

Waombolezaji wakimpa pole.

 

Kada wa CCM na aliyewahi kuwa Mbunge wa Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji (kulia) akiwa na waombolezaji wengine msibani.

PICHA NA AMOS CRISPINE | GLOBAL TV ONLINE