×

Haji Manara Apewa Onyo Kali na TFF

Msemaji wa klabu ya Simba SC ya Dar es salaam, Haji Sunday Manara (katikati) akitolewa nje na polisi.

 

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, imempa onyo kali Msemaji wa klabu ya Simba SC ya Dar es salaam, Haji Sunday Manara kwa kosa la kuingia uwanjani.

 

Kiongozi huyo alifanya kosa hilo Jumapili iliyopita wakati wa mechi ya watani wa jadi ambapo Simba aliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga.

 

Katika barua hiyo iliyotolewa imemtahadharisha kiongozi huyo kwa kuendelea kufanya matukio mengine kama hayo na endapo ataendelea kamati hiyo itachukua hatua kali za kinidhamu dhidi yake. Soma barua hiyo hapa chini: