
HATIMAYE timu zinazotinga fainali ya NBA zimeshafahamika baada ya juzi Warriors na Cavaliers kushinda michezo yao ya kanda.
Hii ni mara ya nne mfululizo timu hizo zin a k u t a n a k w e n y e fainali ya NBA na k u o n g e z a upinzani mkali kwa mwaka huu.
Baada ya timu kumaliza michezo sita kwa sare ya 3-3, Golden State Warriors walifanya maajabu baada ya kuwachapa Houston Rockets kwa pointi 101- 92 na kutinga fainali kwa ushinda wa 4-3.
Awa l i i l i k u w a haiaminiki kama timu hizo zingekwenda fainali tena mwaka huu kutokana na upinzani waliokutana nao kutoka kwenye kanda zao a m b a p o wote walifika kwenye mchezo wa sita wakiwa sare ya 3-3.
Golde n S t a t e w a l ionekana kama vile wangepoteza mchezo huo baada ya kwenda mapumziko wakiwa wamechapwa 54- 43.
Hata hivyo, staa wao Stephen Curry aliamka tena kama ilivyo kawaida yake na kufanikiwa kufunga pointi 14 kati ya 27 alizofunga kwenye mchezo ule.
Hii ina maana sasa Golden State watakwenda tena kwenye ukumbi wa Bay Area kwa mara yao ya nne k u w a a l i k a Cleveland Cavaliers kwenye mchezo wa kwanza wa fainali ambayo itaanza kesho.
Katika mara tatu ambazo wamekutana huko nyuma, Golden State wamefanikiwa kutwaa ubingwa huo mara mbili, huku Cleveland wakitwaa mara moja.
Sasa ni wakati wa Cleveland ambao wamekuwa wakionyesha kiwango cha juu kwa miaka ya hivi karibuni kuhakikisha kuwa wanatwaa ubingwa huo kuanzia wanapoanza harakati za kuutafuta kesho.