Mkuu wa mkoa wa Tabora amenazisha kampeni yake ya ‘JIONGEZE’ maalum kwa ajili ya kupunguza vifo vya mama na mtoto mkoani humo.
RC Mwanri amesema vifo vingi vya wajawazito Tabota vinasababishwa na uzembe wa Madaktari hivyo ametoa maagizo kuwa kila Daktari avae kitambulisho kinachoonesha jina lake ili atakapomfanyia unyama mama mjamzito aweze kumjua jina lake na kutoa rai kwa wakinamama kuwa watakapofanyiwa ukatili na madaktari watoe taarifa na atazishugulikia haraka iwezekanavyo.
