×

MWILI WA KIBONDE WAAGWA MWANZA, KUZIKWA JUMAMOSI – PICHA

Mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Clouds Media Group, Ephraim Kibonde utawasili leo usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JKNIA) na utapelekwa Hospitali ya Jeshi, Lugalo kuhifadhiwa. Taratibu za mazishi zitafanyika nyumbani kwake Mbezi na Jumamosi, Machi 9, 2019 ambapo ataagwa na kuzikwa.

Baba wa marehemu,  Ephraim, Samson Kibonde,  akifarikijiwa na waombolezaji.

 

Ndugu, jamaa na marafiki wa Kibonde, wameungana na waombolezaji nyumbani kwa wazazi wa marehemu huyo Mbezi-Africana jijini Dar es Salaam.

Hali ilivyo msibani.

Hiyo inafuatia msiba huo uliomkuta mtangazaji huyo aliyepatwa na umauti leo asubuhi alipokuwa jijini Mwanza alipokuwa njiani kutoka mkoani Kagera kumzika bosi wake, Ruge Mutahaba.

Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga,  akiwasili msibani.

 

Tayari watu wa Mwanza wameshatoa heshima za mwisho kwa marehemu Ephrahim Kibonde na tayari mwili unaelekea Airport kuanza safari ya kuelekea jijini Dar es salaam kwaajili ya maziko.

 

Waombolezaji wakifika msibani.
Msafara uliobeba mwili wa rafiki yetu mzee wa mastory ya town Ephraim Kibonde (Kibs) ukiwa unaelekea Airport Mwanza tayari kusafirishwa kuja Dar es salaam. Msiba upo nyumbani kwao Marehemu Mbezi Beach karibu na Mbezi Resort. 
Baba Kibonde akifarijiwa.

 

Mama wa Ephrahim, Bi. Hilda Kibonde,  akilia kwa uchungu.

 

Gadna Habash akifarijiana na mmoja wa waombolezaji.