×

Uwanja wa Simba Waitwa Simba Mo Arena

Wanachama klabu ya Simba wamepitisha rasmi uamuzi wa kuuita uwanja wao Simba Mo Arena badala ya Simba Complex uliopo Bunju.

 

Jina hilo limepitishwa muda mfupi baada ya Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara kufanya harambee isiyo rasmi ya ujenzi wa uwanja huo katika meza kuu na kupata ahadi Sh 55.5milioni.

Baada ya harambee hiyo, wanachama walipitisha jina hilo na kuachana na lile la awali la Simba Complex.

Katika Harambee hiyo, mwenyekiti wa zamani wa Simba, Swedy Mkwabi aliahidi kutoa Sh5 Milioni, Hanspope Zacharia Sh10 Milioni, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson Sh 5 Milioni, kaimu Mwenyekiti, Mwina Kaduguda mifuko 20 ya cement, Salim Abdallah Try again Sh15 Milioni.

 

Wengine ni Seleman Haroub (500,000), MO Dewji 20 milioni wakati Haji Manara alitoa tofali 1000.

Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema, yeye ni shabiki kindaki ndaki wa Simba, ila amekuwa akitamani mafanikio ya klabu hiyo yaonekane pia katika klabu nyingine za soka nchini.

 

Dk Tulia ametamka hayo alipokuwa mgeni rasmi kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo unaoendelea jijini Dar es Salaam.

 

“Klabu ya Simba ni mfano wa kuigwa na klabu za upande wa pili,” alisema Naibu Spika huku baadhi ya mashabiki wakimshangilia na kuitaja klabu ya Yanga.

 

 

Leave a Comment