Faru Fausta (57) ambaye ndiye alikuwa Faru mzee duniani amekufa Ijumaa Desemba 27, 2019.
Faru huyo ambaye alikuwa amehifadhiwa kwenye Banda maalum ndani ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kwa zaidi ya miaka mitatu amefariki kutokana na maradhi.
Faru Fausta alikuwa amehifadhiwa kwenye banda hilo ili kumlinda kuliwa na wanyama wengine hasa fisi kutokana jicho lake moja kutoona .
Kamishna wa uhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Dk Fredy Manongi amethibitisha kifo cha faru huyo.