
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati, Lazaro Nyalandu, amechukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 kwa tiketi ya CHADEMA.
Amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumatano Julai 8, 2020, na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi, katika Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Nyalandu amesema atarejesha umoja wa kitaifa na kuondoa tofauti za kisiasa.
“Jambo la kwanza ni kuhakikisha tunarejesha umoja wa kitaifa. Matumaini ya Watanzania ya udugu, upendano na ushirikiano, na penye lawama tupeleke upendo.
“Wakati naondoka CCM nilisema, ili nchi iwe sawasawa ni lazima serikali, mahakama na bunge viwe huru. Haya mafiga matatu yanatakiwa yajitegemee na yajiendeshe pamoja,” amesema.