
RAIS JohnMagufuli leo Alhamisi, Julai 9, 2020, amewatembelea na kuwapa pole wafiwa nyumbani kwa marehemu Balozi Job Lusinde, Uzunguni, jijini Dodoma.

Lusinde ambaye alikuwa waziri wa Mwl. Nyerere alifariki alfajiri ya Julai 7, 2020, katika Hospitali ya Mloganzira Dar alikokuwa akipatiwa matibabu.
