
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa jukumu la kulainisha mitambo ya uchaguzi kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imekabidhiwa kwa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT).
Amesema hayo wakati akihutubia Baraza Kuu la Wanawake Tanzania (UWT) katika ukumbi wa White House mjini Dodoma, ambapo amesema kuwa jukumu la kampeni ni jukumu zito.

“Jukumu hili ukilichambua kiundani ni jukumu zito sana kujitoa na kujitolea kwa sababu kazi tunayokwenda nayo ya kuanza ya kampeni si kazi nyepesi, ” amesema.
Amesisitiza kuwa inahitaji uadilifu na umakini mkubwa kwani Chama Cha Mapinduzi ni kikubwa na kinahitaji ushindi mkubwa.
