MGOMBEA urais kupitia Chama cha Wananchi( CUF) Profesa Ibrahim Lipumba na mgombea mwenza, Hamida Abdallah Huweishi, leo Agosti 11, 2020, wamechukua fomu za kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), zilizopo Dodoma.
Lipumba na Huaeshi wamekabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa NEC Jaji wa Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage.


