×

Wadau wa Korosho Nchini Waazimia Kupandisha Thamani ya Zao Hilo

Wadau wakiwa makini kwenye warsha hiyo.

Bodi ya Korosho nchini kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo TMX, WHI na nyinginezo kutoka ndani na nje ya nchi leo wamefanya warsha na wadau kujadili jinsi ya kuinua zao hilo hapa nchini. Warsha hiyo imefanyika Jengo la LAPF Milleniun Tower Jijini Dar

Akizungumza kwenye warsha hiyo, Mwenyekiti wa Chama cha Wabanguaji Wakubwa nchini, Bahati Mayoma amesema warsha hiyo imelenga kuinua sekta ya korosho ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu.

Mwenyekiti wa Chama cha Wabanguaji Wakubwa Bahati Mayoma (kulia) akitoa ufafanuzi wa jambo kwenye warsha hiyo.

Mayoma amesema kwa zaidi ya miaka kumi ubanguaji umekuwa chini ya asilimia kumi.

“Hii imepelekea ajira nyingi zilizokuwa zikipatikana kwa kazi ya ubanguaji korosho kupotea.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tanzania Private Sector Foundation, Zachy Mbenna akitoa somo kwenye warsha hiyo.

Korosho ghafi zimekuwa zikipelekwa nje ya nchi ambapo huko wakishazibangua na kuziboresha wanaziweka nembo za nchi zao na kuziuza kwa bei kubwa zaidi”. Alisema Mayoma.

Mayoma aliendelea kusema kuwa malengo ya warsha hiyo waliyowashirikisha wadau kutoka nchi za nje ni kuhakikisha wanabadilishana uzoefu katika uboreshaji wa zao hilo ambalo linazalishwa kwa wingi hapa nchini.

Mhadhiri wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Academy, Geni Kasoga akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kwenye warsha hiyo.

Alimalizia kwa kusema malengo ya warsha hiyo kufikia mwaka 2024 mpaka 2025 nusu ya korosho inayopelekwa nje ya nchi iwe inabanguliwa hapa nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tanzania Private Sector Foundation, Zachy Mbenna amesema zao hilo hapa nchini linakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya bilioni 250 za Kimarekani na kuwataka wadau kuamka nalo ambapo linaonekana kama limesakusahaulika.

Mwalimu na mwezeshaji wa kilimo cha kisasa, Adam Ngamange (kushoto) akifuatilia jambo kwenye warsha hiyo.

“Hili zao tukiwa nalo makini litawainua wadau kama Tanzanite yetu ilivyomuinua mchimbaji mdogo hapa nchini baada ya kuipa umuhimu sekta ya madini kufikia hatua ya kuuzunguushia ukutani mgodi wa madini hayo”. Alisema Mbenna.

Wengine waliochangia mada mbalimbali kwenye warsha hiyo ni pamoja na Mhadhiri kutoka Chuo cha Mwalimu Nyerere Academy Dkt. Geni Kasoga, Mkurugenzi wa Soko la Bidhaa nchini, Agustino Mburumi na wengineo.

Bango la Bodi ya Korosho.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                       HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL        

Leave a Comment