
Aliyekuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amezuiwa kutoka Tanzania kupitia mpaka wa Namanga.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, Nyalandu ambaye amewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii hakuwa na nyaraka muhimu.
Amesema, Maafisa wa Uhamiaji wamemzuia kuondoka huku baadhi ya vitu alivyotaka kusafirisha vikishikiliwa mwanasiasa huyo ametakiwa kuwasilisha nyaraka husika na atafikishwa Mahakamani endapo atashindwa kufanya hivyo.