
Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) anayedaiwa kumpiga mwaamuzi Fadhil Maka aliyekuwa akichezesha mchezo kati ya Pamba FC na Rhino Rangers juzi tarehe Desemba 5, 2020 katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza, amekamatwa na Jeshi la polisi mkoani humo kwa kitendo hicho.
Kamanda wa Polisi Mwanza, ACP. Muliro Jumanne amesema askari huyo atashughulikiwa sawa na wahalifu wengine.