
Mwili wa Baba Mzazi wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Jokate Mwegelo, leo uliagwa na waombolezaji kwenye ibada iliyofanyika Kanisa la St. Peters Jijini Dar na hatimaye kusafirishwa kuelekea Mbinga mkoani Ruvuma.
Katika ibada hiyo ndugu jamaa na marafiki walitoa heshima zao za mwisho kwa marehemu na hatimaye msafara mazishi ulianza safari ya kuelekea Mbinga.





