
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella ameamuru kukamatwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema, Boniface Magesa, na afisa ardhi wake kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo kwa mkuu wa wilaya ya Sengerema na mkuu huyo wa mkoa.
Mongella ametoa amri hiyo muda mfupi baada ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo kusikiliza kilio cha mkazi wa Sengerema, Christopher Derefa, aliyedai kudhulumiwa fedha za malipo ya fidia.