×

JPM Asali Ibada Ya Jumapili Kanisa La Bikira Maria Chato, Geita

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli leo Januari 17, 2021 wameungana na Waumini wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria, Parokia ya Chato Mkoani Geita kusali Misa Takatifu (Dominika ya 2 ya Mwaka B) iliyoongozwa na Paroko wa Parokia hiyo, Padre Henry Mulinganisa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakijumuika na waumini wengine wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato katika Ibada ya Jumapili ya Dominika ya pili iliyofanyika Chato mkoani Geita leo tarehe 17 Januari 2021.
Rais Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakishiriki Sakramenti Takatifu katika Ibada.
Rais Magufuli akizungumza na Waumini wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato katika Ibada.
Rais Magufuli akimshukuru Paroko wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Padre Henry Mulinganisa mara baada ya kuzungumza na Waumini wa Kanisa hilo Chato mkoani Geita.
Rais Magufuli akiwasalimia Masista mara baada ya Ibada.
Rais Magufuli akiwasalimia Vijana wadogo wa Kikatoliki mara baada ya Ibada.
Rais Magufuli akiwa katika picha na Paroko wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Padre Henry Mulinganisa pamoja na Vijana wa Kikatoliki.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimsalimia Paroko wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Padre Henry Mulinganisa mara baada ya Ibada Kanisani hapo.

Leave a Comment