


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa, na Naibu wake Mhe. Abdallah Ulega, jana Machi 11, 2021 jijini Dodoma wamekutana na menejimenti ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dkt. Ayub Rioba Chacha.
Katika kikao hicho pamoja na mambo mengine kilijadili maendeleo ya Shirika hilo katika kutoa habari kwa wananchi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa studio za televisheni ya Shirika hilo zilizopo Mikocheni Jijini Dar es Salaam na Ujenzi wa studio ya Redio Jamii makao makuu jijini Dodoma.