×

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Rais wa China

RAIS Samia Suluhu Hassan, leo Juni 21, 2021 amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping.

 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu, katika mazungumzo hayo, Tanzania na China zimekubaliana kukuza ushirikiano katika nyanja za uchumi, utamaduni na ushirikiano wa kimataifa.

 

 

Pia China imeahidi kufungua zaidi soko lake kwa bidhaa za Tanzania pamoja na kuongeza uwekezaji hususan katika sekta ya viwanda.

 

 

Leave a Comment