Watu wengi huamini kwamba mtoto akizaliwa na ulemavu, basi hawezi kuwa na uwezo wowote wa kufanya mambo makubwa maishani mwake na wengi huchukuliwa kama mizigo, huku jamii nyingine zikiwa na imani potofu kwamba kuzaa mtoto mwenye ulemavu ni laana.
Hata hivyo, Zion Clark aliyezaliwa bila miguu, ameuthibitishia ulimwengu kwamba kuzaliwa na ulemavu siyo kikwazo kabisa katika maisha na kuonesha kwamba kumbe hata walemavu, wanaweza kufanya mambo makubwa na kuweka rekodi ambazo haziwezi kusahaulika duniani.