
NI headlines kutoka kwa mpiga picha maarufu wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Lukamba ambaye amefuta utambulisho uliokuwa ukimtambulisha kama mpiga picha rasmi (official photographer) wa msanii Diamond katika ukurasa wake wa Instagram.
Kwa sasa ukipitia ukurasa wake wa Instagram, Lukamba amejitambulisha kama mwongozaji wa filamu (film director) jambo ambalo limeacha maswali kwa baadhi ya mashabiki.
Hata hivyo Katika kipindi cha hivi karibuni kumekua na taarifa za mpiga picha huyo kufutia kazi na mwanamuziki #diamondplatnumz kabla ya kuonekana tena kwa pamoja katika ziara ya kimuziki ya msanii huyo nchini Marekani.