
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa wanahabari na wafiwa wote kutokana na ajali iliyotokea leo katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu na kusababisha vifo vya watu 14 wakiwamo waandishi wa habari sita.
Mkuu huyo wa nchi ametuma salama hizo leo Jumaane Januari 11, 2022 akisema amestushwa na vifo hivyo vilivyotokea baada ya gari ya waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria aina ya Toyota Hiace .
Katika ukurasa wake wa Tweeter Rais Samia amesema “Nimeshtushwa na vifo vya Watu 14 wakiwemo Wanahabari 6 vilivyotokea leo asubuhi baada ya gari lililokuwa katika msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kugonga na Daladala. Poleni Wafiwa, Wanahabari na jamaa wote. Mungu aziweke mahali pema roho za Marehemu na Majeruhi wapone haraka”