×
Global Publishers
  • Home
  • Habari
    • Kimataifa
    • Kitaifa
  • Global TV
  • Magazeti
  • Ajira
  • Burudani
    • Audio Music
    • Music Videos
    • Dar Live
  • Michezo
  • Makala
    • Afya
    • Mahaba & Maisha
    • Burudani
    • Hadithi
    • Mikasa
    • Siasa
  1. Home
  2. Habari
  3. Mtuhumiwa wa Mauaji Azidiwa Kizimbani, Jaji Aahirisha Kesi

Mtuhumiwa wa Mauaji Azidiwa Kizimbani, Jaji Aahirisha Kesi

Global Publishers January 15, 2022 4,556 views 0 Comments
SHARE THIS:

Kesi ya mauaji inayomkabili Timothy Gitonga mwenye umri wa miaka 30, anayetuhumiwa kumuua bibi yake, Journes Kiringa mwenye umri wa miaka 80, imeshindwa kusikilizwa kufuatia mtuhumiwa huyo kuzidiwa na maradhi akiwa kizimbani.

 

Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa katika Mahakama ya Embu, nchini Kenya ambapo mtuhumiwa alipoingizwa mahakamani, alianza kulalamikia maumivu makali aliyokuwa akiyahisi, jaji akaamuru kesi iendelee lakini mtuhumiwa aliendelea kulalamikia maumivu makali huku akionesha kuzidiwa.

 

Kufuatia hali hiyo, Jaji Tony Kwambai aliamua kusitisha usikilizwaji wa kesi hiyo na kuagiza mtuhumiwa apelekwe katika Hospitali ya Embu na baada ya matibabu arejeshwe katika Kituo cha Polisi Itabua kisha apelekwe tena mahakamani hapo ifikapo Januari 17, mwaka huu.

 

Mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kudaiwa kumshambulia bibi yake na kumuua huku akimjeruhi vibaya babu yake, Jamleck Wamai ambaye anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Embu.

 

Tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Rungana, Nembure ambapo sababu za tukio hilo hazijafahamika na baada ya kutenda ukatili huo, mtuhumiwa alitoroka kabla ya kukamatwa na polisi.

SHARE THIS:
Previous Next

Related Posts

Simba Yatenga Sh Milioni 600 Za Usajili - Global Publishers CHAMPIONI

Simba Yatenga Sh Milioni 600 Za Usajili

May 31, 2017
VIDEO: Magufuli Aagiza Mahabusu Wanaoshikiliwa Kimakosa Waachiwe - Global Publishers HABARI

VIDEO: Magufuli Aagiza Mahabusu Wanaoshikiliwa Kimakosa Waachiwe

July 18, 2019
Absa Bank Tanzania Yafunga Kampeni Ya ‘Ujanja Ni Kuswipe Na Kadi Ya Absa’ Kwa Droo Ya Mwisho Na Kutangazwa Kwa Mshindi Wa Zawadi Kuu - Global Publishers HABARI

Absa Bank Tanzania Yafunga Kampeni Ya ‘Ujanja Ni Kuswipe Na Kadi Ya Absa’ Kwa Droo Ya Mwisho Na Kutangazwa Kwa Mshindi Wa Zawadi Kuu

January 18, 2026
Kinana Akutana na Balozi wa Marekani, Uhusiano Kati ya Tanzania na Marekani Kuimarishwa - Global Publishers HABARI

Kinana Akutana na Balozi wa Marekani, Uhusiano Kati ya Tanzania na Marekani Kuimarishwa

April 11, 2022

Leave a Comment Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

DAKTARI

GLOBAL TV Online




SIMBA
YANGA
NEWS
Global Publishers
  • About Us
Download on the App Store
Get it on Google Play

© 2026 Global Publishers. All Rights Reserved.

Designed by Yatosha Web Services