×
Global Publishers
  • Home
  • Habari
    • Kimataifa
    • Kitaifa
  • Global TV
  • Magazeti
  • Ajira
  • Burudani
    • Audio Music
    • Music Videos
    • Dar Live
  • Michezo
  • Makala
    • Afya
    • Mahaba & Maisha
    • Burudani
    • Hadithi
    • Mikasa
    • Siasa
  1. Home
  2. Habari
  3. Mtuhumiwa wa Mauaji Azidiwa Kizimbani, Jaji Aahirisha Kesi

Mtuhumiwa wa Mauaji Azidiwa Kizimbani, Jaji Aahirisha Kesi

Global Publishers January 15, 2022 0 Comments
SHARE THIS:

Kesi ya mauaji inayomkabili Timothy Gitonga mwenye umri wa miaka 30, anayetuhumiwa kumuua bibi yake, Journes Kiringa mwenye umri wa miaka 80, imeshindwa kusikilizwa kufuatia mtuhumiwa huyo kuzidiwa na maradhi akiwa kizimbani.

 

Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa katika Mahakama ya Embu, nchini Kenya ambapo mtuhumiwa alipoingizwa mahakamani, alianza kulalamikia maumivu makali aliyokuwa akiyahisi, jaji akaamuru kesi iendelee lakini mtuhumiwa aliendelea kulalamikia maumivu makali huku akionesha kuzidiwa.

 

Kufuatia hali hiyo, Jaji Tony Kwambai aliamua kusitisha usikilizwaji wa kesi hiyo na kuagiza mtuhumiwa apelekwe katika Hospitali ya Embu na baada ya matibabu arejeshwe katika Kituo cha Polisi Itabua kisha apelekwe tena mahakamani hapo ifikapo Januari 17, mwaka huu.

 

Mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kudaiwa kumshambulia bibi yake na kumuua huku akimjeruhi vibaya babu yake, Jamleck Wamai ambaye anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Embu.

 

Tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Rungana, Nembure ambapo sababu za tukio hilo hazijafahamika na baada ya kutenda ukatili huo, mtuhumiwa alitoroka kabla ya kukamatwa na polisi.

SHARE THIS:
Previous Next

Related Posts

Waziri Mkuu Atoa Wito kwa DAWASA Kuendelea Kutafuta Vyanzo Vipya vya Maji - Global Publishers HABARI

Waziri Mkuu Atoa Wito kwa DAWASA Kuendelea Kutafuta Vyanzo Vipya vya Maji

November 29, 2022
WEMA: Nilikuwa Namsubiri kwa Hamu VAN VICKER – Video - Global Publishers HABARI

WEMA: Nilikuwa Namsubiri kwa Hamu VAN VICKER – Video

September 27, 2018
Uwoya Asakwa Kwa Kifo cha Bodaboda - Global Publishers BURUDANI

Uwoya Asakwa Kwa Kifo cha Bodaboda

March 16, 2017
LSF na Mpango wa Uwezeshaji Wanawake Kutambua Haki Zao Kiuchumi - Global Publishers HABARI

LSF na Mpango wa Uwezeshaji Wanawake Kutambua Haki Zao Kiuchumi

November 5, 2021

Leave a Comment Cancel reply

You must be logged in to post a comment.



DAKTARI

GLOBAL TV Online




SIMBA
YANGA
NEWS
Global Publishers
  • About Us
Download on the App Store
Get it on Google Play

© 2026 Global Publishers. All Rights Reserved.

Designed by Yatosha Web Services