
KIKOSI cha Yanga, kimeitengea Mtibwa Sugar siku 15 za kuhakikisha zinaibuka na ushindi katika
mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa Februari 23, mwaka huu kwenye Uwanja wa Manungu,
Morogoro.
Yanga wametamba kuwamaliza Mtibwa wakiwa kwao huku wakiwa na kumbukumbu ya kuishuhudia Simba
ikitoka suluhu ilipokwenda kucheza huko hivi karibuni.
Katika msimamo wa Ligi Kuu Bara hivi sasa, Yanga wanaongoza wakiwa na pointi 36, huku Mtibwa ikiwa na pointi 12 katika nafasi ya 14. zote zimecheza mechi 14.
Akizungumza na Championi Jumatano, Winga wa Yanga, Dickson Ambundo, amesema: “Maandalizi yetu
yapo vizuri kuelekea mchezo huo, tumepata muda wa kupumzika wa kutosha, sasa ni muda wa kujipanga kuwamaliza Mtibwa.
“Kwaupande wangu nimejipanga kupambana kwa hali ya juu ili kuweza kuisaidia timu yangu kupata matokeo
mazuri, ukiangalia tulipata matokeo ya sare kwa mchezo uliopita na mchezo huu tunataka matokeo ya ushindi.
Stori: Careen Oscar, Dar es Salaam