×

Rais Samia Aelekea Nchini Marekani kwa Ziara ya Kikazi Asubuhi ya Leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiagana na Makamu wa Rais,  Dkt. Philip Mpango katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam wakati akielekea nchini Marekani kwa ziara ya kikazi.

Rais Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Aprili 13, 2022 kwenda Marekani kwa ziara ya kikazi. Pamoja na mambo mengine anatarajiwa kushiriki uzinduzi wa filamu ya ‘Tanzania Royal Tour’ itakayozinduliwa Aprili 18, 2022 jijini New York.

Leave a Comment