
Viongozi wa Ufaransa na Ujerumani wamemhimiza Vladimir Putin wa Urusi kufanya mazungumzo ya moja kwa moja mazito na rais wa Ukraine, ofisi ya kansela wa Ujerumani ilisema Emmanuel Macron na Olaf Scholz walizungumza na Bw Putin kwa simu kwa dakika 80.
Wawili hao walisisitiza kusitishwa kwa mapigano mara moja na kuondolewa kwa wanajeshi wa Urusi, ofisi ya kansela ilisema.Kiongozi wa Urusi alisema Moscow iko tayari kuanza tena mazungumzo na Kyiv, kulingana na Kremlin.
Haikutaja uwezekano wa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Bw Putin na mwenzake wa Ukraine, Volodymyr Zelensky.
Rais wa Ukraine hapo awali alisema hakuwa na shauku ya mazungumzo, lakini akaongeza kuwa kuna uwezekano wa kuhitajika kumaliza mzozo huo.
Wajumbe wa Urusi na Ukraine wamefanya duru nyingi za mazungumzo kwa mbali na ana kwa ana tangu Urusi ilipovamia tarehe 24 Februari, lakini juhudi zimekwama hivi karibuni.
Ufaransa na Ujerumani pia zilimtaka Bw Putin kuwaachilia huru wapiganaji 2,500 wa Ukraine waliochukuliwa kama wafungwa wa vita katika kiwanda cha kutengeneza chuma cha Azovstal huko Mariupol.
Kiwanda hicho kilichokuwa kinasambaa kilikuwa cha mwisho katika mji wa bandari wa kusini, ambao ulistahimili mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa vikosi vya Urusi na sasa ni magofu.