×

Rais wa Yanga Akabidhi Kadi za Uanachama kwa Wanandoa Wapya Nandy na Billnass

Rais wa Yanga Injinia Hersi (katikati) akiwa na wanandoa Wapya Nandy na Billnass

RAIS  wa klabu ya Yanga Injinia Hersi Said jana amekabidhi kadi za uanachama kwa Wasanii Faustina Mfinanga Maarufu Nandy na William Lyimo ambao jana walifunga pingu za Maisha.

 

Mbali na kadi hizo pia Injinia Hersi aliwakabidhi fedha  Tsh Mil 5, Rais huyo ambaye alichaguliwa hivi karibuni alikuwa mmoja ya watu maarufu waliohudhuria sherehe  ya mastaa hao wa bongo fleva iliyofanyika Mlimami City, Dar es salaam.

 

Nandy na Billnass wamefunga pingu ya maisha katika  hii kanisa la KKKT Ushirika wa Mbezi Beach Dar Es Salaam na kuhudhuriwa na ndugu jamaa na marafiki.

Leave a Comment