×
Global Publishers
  • Home
  • Habari
    • Kimataifa
    • Kitaifa
  • Global TV
  • Magazeti
  • Ajira
  • Burudani
    • Audio Music
    • Music Videos
    • Dar Live
  • Michezo
  • Makala
    • Afya
    • Mahaba & Maisha
    • Burudani
    • Hadithi
    • Mikasa
    • Siasa
  1. Home
  2. Habari
  3. Waziri Mkenda: RUWASA Ijitathmini Inamhujumu Waziri Aweso Usimamizi wa Maji Rombo

Waziri Mkenda: RUWASA Ijitathmini Inamhujumu Waziri Aweso Usimamizi wa Maji Rombo

Global Publishers July 29, 2022 0 Comments
SHARE THIS:
Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) umetakiwa kujitathmini kutokana na kadhia ya kushindwa kusimamia mradi wa maji Wilayani Rombo.
Mbunge wa Jimbo la Rombo ambaye pia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prf Adolf Mkenda ametoa kauli hiyo tarehe 26 Julai 2022 wakati akiwa katika muendelezo wa ziara jimboni humo ambapo amekagua ujenzi wa mradi wa maji wa Bilioni 2.9
Prof Mkenda amekagua mradi huo ambao mkandarasi alisaini kuanza kazi mwanzoni mwa mwaka huu 2022 lakini mpaka sasa hakuna kazi iliyokwisha kufanyika zaidi ya kuwekwa mchanga na kokoto zisizozidi hata gari moja.
Prof Mkenda amesema kuwa ameamua kufika na kukagua chanzo cha maji katika mto Wona ambapo mradi huo utakapokamilika utarahisisha upatikanaji maji kwa lita Milioni 4 kwa siku na kupunguza kwa kiasi kikuwa tatizo la maji Rombo linaloikabili Wilaya ya Rombo.
“Tatizo namba moja, mbili, na tatu Rombo ni maji sasa mtu anayechezea mradi wa maji sielewi ana madhumuni gani na anataka wananchi wa Rombo wawe na taswira gani kwa serikali, wanamhujumu Waziri wa Maji Mhe Juma Aweso ambaye ni mchapakazi na kwa hili nitamualika aje aone changamoto hii” Amekaririwa Prof Mkenda
Amesema kuwa Mradi huo ni sehemu ya miradi ya maji yenye jumla ya Bilioni 10 iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya maji Wilayani Rombo.
“Kwa kuwa sehemu hiyo ni ngumu kufika sio rahisi kwa viongozi kufika na kuona maendeleo ya mradi huo inakuwa rahisi kuficha mapungufu haya kwahiyo RUWASA inabidi ijiangalie upya kwa kuwa ndio msimamizi wa mradi huo” Amesisitiza Prof Mkenda
Mhe Prof Adolf Mkenda ambaye ni mbunge wa Jimbo la Rombo Mkoani Kilimanjaro amesema kuwa kwa sasa katika Wilaya ya Rombo, RUWASA inatia shaka usimamizi wake wa miradi ya maji hvyo amemuomba Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mhandisi Clement Kivegalo kutembelea Rombo ili kujionea kadhia hiyo ya ucheleweshwaji wa mradi wa maji.
Na Mathias Canal, Rombo
SHARE THIS:
Previous Next

Related Posts

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano June 28, 2017 - Global Publishers HABARI

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano June 28, 2017

June 28, 2017
Waziri Mkuu Akabidhi Mil 400/= Kutoka NMB Kuchangia Akina Mama Wenye Fistula - Global Publishers HABARI

Waziri Mkuu Akabidhi Mil 400/= Kutoka NMB Kuchangia Akina Mama Wenye Fistula

September 27, 2021
Stanbic Yaendeleza Ukuaji wa Biashara kwa Watanzania Kwenye Sekta ya Madini - Global Publishers HABARI

Stanbic Yaendeleza Ukuaji wa Biashara kwa Watanzania Kwenye Sekta ya Madini

June 15, 2025
Waziri Mkuu Majaliwa Afungua Kikao Kazi Cha TRA, Ahimiza Tathmini Na Uboreshaji Wa Utendaji - Global Publishers HABARI

Waziri Mkuu Majaliwa Afungua Kikao Kazi Cha TRA, Ahimiza Tathmini Na Uboreshaji Wa Utendaji

July 8, 2025

Leave a Comment Cancel reply

You must be logged in to post a comment.



DAKTARI

GLOBAL TV Online




SIMBA
YANGA
NEWS
Global Publishers
  • About Us
Download on the App Store
Get it on Google Play

© 2026 Global Publishers. All Rights Reserved.

Designed by Yatosha Web Services