MABINGWA watetezi wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara, Yanga SC wameanza kampeni za kuutetea ubingwa wao kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Polisi Tanzania katika dimba la Sheikh Amri Abeid Arusha.
Yanga walilazimika kutoka nyuma 1-0 na kushinda 2-1 kwa magoli ya Fiston Mayele na nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto.
POLISI TZ 1-2 YANGA SC
⚽ Kipemba 34′
⚽ Mayele 42′
⚽ Mwamnyeto 85′
