×

Mawakala Wa Utalii Waanza Kumiminika Nchini Kuangalia Vivutio Vya Utalii Na Kwenda Kuvitangaza

Mawakala hao wakiwasili hapa nchini.

Katibu Mkuu  Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Eliamani Sedoyeka jana aliongoza mapokezi ya Mawakala hao kutoka katika masoko ya kimkakati katika nchi tofauti. Nchi walizotoka Mawakala hao ni Marekani, Canada, Mexico, Ubelgiji na Brazil.

Wadau katika picha ya pamoja.

Akizungumza mara baada  ya kuwapokea Mawakala hao, Prof. Sedoyeka amesema “Leo tumeanzisha Mega Trip ambayo kwa kawaida Wizara kupitia Bodi ya Utalii ( TTB) uandaa safari kama hizi ambazo uwaleta waongoza Utalii,  Waandishi wa Habari na wadau wakuu wa utalii wa kimkakati ili waje Tanzania kuangalia maeneo yetu mbali mbali ya vivutio”.

Ulipofika muda wa msosi.

Sedoyeka amesema watalii wanavyokuja nchini uletwa na makampuni ambayo tayari kama nchi imeshawajengea uwezo Mawakala wa nchi hizo juu  ya vivutio vilivyopo nchini.

“Ziara hii inakuja baada ya Wizara ya Maliasili na Utalii  kuwa na mashirikino mazuri na kampuni ya Ndege ya Qatar na pia ni muendelezo wa matunda ya Royal Tour iliyoongozwa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Amesema Sedoyeka.

Amesema, Tanzania imeingia makubaliano ya kimkakati  kuanzisha mahusiano ya  kibiashara ili kuwatangazia duniani kuwa Tanzania kuna  vivutio vya aina gani, mahusiano ya kimkakati ili kumtengenezea mtiririko wa wageni.

Amesema, kufunguka kwa masoko ya kimataifa yanasaidia kukua kwa uchumi wa nchi na kuongezeka kwa pato la taifa. Wafanyabiashara wanapata fedha.

Leave a Comment