
Shangazi yake Suleman Dawood, ambaye alikuwa kwenye nyambizi ya Titan chini ya maji na baba yake Shahzada, anasema kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa anasitasita kuhusu safari ya kwenda kuona ajali ya Titanic siku zilizopita.
Akizungumza na NBC News, Azmeh Dawood, dada yake Shahzada, alisema Suleman alimwambia kwamba alihisi “kuogopa” kuhusu safari hiyo, lakini alitaka kumfurahisha baba yake.
Walipanda nyambizi hiyo Jumapili iliyopita, ambayo ilikuwa Siku ya Akina Baba huko Amerika Kaskazini.
“Siamini kilichotokea,” Azmeh alisema.”Ni hali ya kushangaza.”
“Ninahisi kama nimenaswa katika hali hatari sana, na muda unayoyoma, lakini haujui utafanya nini kujinusuru,” alisema. “Mimi binafsi napata tabu kupumua nikiwafikiria.”