
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye siku muhimu kwa Klabu ya Simba (Simba Day) itakayofanyika Jumapili, Agosti 6, 2023.
Klabu ya Simba imemshukuru Dkt Samia kwa mchango wake mkubwa kwenye sekta ya Michezo na Maendeleo ya Taifa kwa ujumla na kumkaribisha kwenye tukio hilo muhimu kwa wapenda michezo wote nchini Tanzania.
