
Mshambuliaji, Neymar Jr amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na miamba ya Saudi Arabia, Al Hilal kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 90 kutoka Paris Saint-German.
Neymar (31) raia wa Brazil amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia klabu hiyo mpaka Juni 2025 na atalipwa mshahara wa Euro milioni 150 (≈ Tsh bilioni 410).
