Rais Samia Afungua Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (Picha +Video)
Global Publishers August 21, 2023 0 Comments
SHARE THIS:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipokea Shada la maua kutoka kwa mtoto Evynne Anicet Maganya (9) Mkazi wa Arusha, wakati alipowasili katika Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha kwa ajili ya kufungua Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya Kanisa hilo tarehe 21 Agosti, 2023
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Agosti 21, 2023 amefungua Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya Kanisa ya kanisa la KKKT Arusha.
Rais Samia Suluhu Hassani ameombwa Bajaji na mlemavu mmoja jijini Arusha kwa lengo la kujikimu kimaisha.
Rais Samia akisalimiana na Maaskofu na Viongozi mbalimbali wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wakati alipowasili katika Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha kwa ajili ya kufungua Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya Kanisa hilo tarehe 21 Agosti, 2023Rais Samia akifungua kitambaa pamoja na Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kuashiria ufunguzi rasmi wa Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yaliyofanyika katika Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha tarehe 21 Agosti, 2023Rais Samia akikata utepe pamoja na Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kuashiria ufunguzi rasmi wa Maabara za Sayansi za Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yaliyofanyika katika Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha tarehe 21 Agosti, 2023