
Rais Samia amemteua Balozi Prof. Kennedy Godfrey Gastorn kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Dkt. Evaristo Longopa aliyeteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu
Pia, Rais amemteua Balozi Stephen Patrick Mbundi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje anayeshughulikia Mambo ya Afrika Mashariki
Aidha, Balozi Said Shaibu Mussa ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akichukua nafasi ya Balozi Fatma Rajab aliyeteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania – Qatar
