
Mama’s Day Out Beach Party wameadhimisha siku ya Afya ya akili kwa kuwakutanisha kina mama 170 Jijini Dar es Salaam katika
Kongamano lililoandaliwa na Kampuni ya Ekima
Insights inayoongizwa Mkurugenzi wake ambaye ni Mwanahabari mkongwe Marion Elius .
Kongamano hilo linefanyika hivi karibuni katika ufukwe Uninio Jijini Dar es Salaam.

“Mama’s day Out Beach Party imefanyika kwa mara ya pili sasa ambapo tulianza mwaka jana 2022 huku lengo letu kubwa ni kutoa elimu
ya kina kuhusu Afya ya Akili katika jamii yetu kwa kupitia wanawake kwa sababu hivi sasa kumekua changamoto katika maeneo mbalimbali ya maisha yetu ya kila siku” amesema Marion.
Mkurugezi huyo amesema kuwa kongamano hil limefanyika sambamba na
maadhimisho ya Wiki ya Afya ya Akili ambayo huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 10 ya kika mwaka huku kauli mbiu yake ikiwa ni #Jikubali #AnzaUpya. #PendaMaisha” amesema Marion.

Amesema kuwa katika kongamano hilo kulikuwa na watoa mada mbalimbali amewataja baadhi yao kuwa ni Mwanasaikolojia maarufu Dkt. Chris Mauki na wataalamu wabobevu katika masuala ya Afya ya Akili ambao wametoa mada mbalimbali akiwamo
Bi Caroline Mwanri , aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communication na Afisa
Rasilimali watu Francis Nanai ambaye amezungumza na kuwapa mbinu wanawake juu ya suala zima la kujiimarisha kiuchumi na namna ya utunzaji wa fedha kuwekeza na pia kujiandaa na maisha ya kustaafu kwani kumekuwa na wimbi kubwa la wastaafu wengi kupoteza mwelekeo kwa sasa kuwa watanzania wengi hawana elimu ya kujiandaa na kustaafu ambayo imekuwa
ikipelekea watu kupata msongo wa mawazo pindi wanapostaafu.
Mwanasaikolojia
Dkt. Chris Mauki ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam amesema kuwa wanawake wanauwezo mkubwa wa kuilewa saikologia ya mwanaume na kumudu kuwasaidia afya yao ya akili na kukuza uwezo vijana wa kiume katika.

Aidha Mwanamtindo na mbunifu wa mitindo ya mavazi kutoka Kampuni ya J’adore Ruth Urio amesema kuwa wanawake wapunguze kuwa na fikra zinazowapotezea muda wa kufanya masuala ya maendeleo yao na jamii kwa ujumla.
Katika kongamano hilo mgeni rasmi alikuwa Diwani kata ya Kunduchi Mhe. Michael Urioh ambaye amewasisitiza kina mama hao umuhimu wa wanawake kuwa wananafasi kubwa katika malezi ya familia na hasa ikizingatiwa tuko kwenye nyakati ambazo kuna muingiliano wa kimaadili na tamaduni toka
nchi za ng’ambo, hivyo ni muhimu sana kwa wanawake kuwa jasiri
na thabiti katika malezi hasa ikizingatiwa
kuwa kuna ongezeko kubwa sana la
watoto kulelewa na mzazi mmoja ambao wengi wao ni wanawake.
Mhe Urioh amesema kuwa serikali chini ya uongozi wa Rais wetu Mama
yetu Samia Suluhu Hassan imejikita katika kumuinua mwanamke katika
maeneo mbali mbali na hasa kupatiwa mikopo isiyokuwa na riba na
kuhamasisha wanawake kujitokeza kutumia kikamilifu fursa hizo.
Kongamano hilo limenogeshwa na michezo mbalibali kama vile kuvuta kamba, kuvumbua dhahabu huku wakipata zawadi kutoka kwa Shear Illusion, GSM, J’Adore, Renex, Cassandra
lingerie The Deck Resturant .
Aidha muandaaji ametoa shukran kwa Taasisi ambazo waneshiriki kikamilifu ambao ni Hospitali ya Kairuki Memorial ya Mikocheni
Dawasa, Coca-Cola Kwanza, Vodacom, GSM, Renex,
J’Adore na wengine wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.