
MAGOLI yaliyofungwa na Jonathan Sowah wa Medeama na Pacome Zouzoua wa Yanga yameziwezesha timu hizo kutoka sare ya goli 1-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Kundi D uliopigwa kwenye Uwanja wa Kumasi Nchini Ghana
Mchezo mwingine wa Kundi hilo AlAhly ya Misri imepata matokeo ya 0-0 dhidi ya CBelouizdad yaAlgeria
Baada ya mechi hizo, Al Ahly inaongoza ikiwa na pointi 5, CR Belouizdad (4), Medeama (4) na Yanga ina (2)
Michezo inayofuata Belouizdad itaikaribisha Al Ahly (Desemba 19, 2023), Yanga itakuwa mwenyeji wa Medeama (Desemba 20, 2023)
FT: MEDEAMA 🇬🇭 1-1 🇹🇿 YANGA SC
⚽ Sowah ( P) 26’
⚽ Zouzoua 36’
FT: Al Ahly 🇪🇬 0-0 🇩🇿 CR Belouizdad
MSIMAMO KUNDI D
1. 🇪🇬 Al Ahly (pointi 5)
2. 🇬🇭 Medeama (4)
3. 🇩🇿 CR Belouizdad (4)
4. 🇹🇿 Yanga SC (2)
Kuna tofauti ya alama tatu kati ya kinara Al Ahly ya Misri na washika mkia Young Africans SC, bado nafasi ipo.