
Treni ya Umeme ya Kisasa (SGR) leo Februari 26, 2024 imepita maeneo ya Pugu Jijini Dar es Salaam katika majaribio yake ya kawaida. Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeanza majaribio ya Treni hiyo ya SGR kutoka Mkoani Dar es Salaam hadi Mkoani Pwani na hivi karibuni itaendelea na majaribio hayo mpaka Mkoani Morogoro. Huduma rasmi za Usafiri huo zinatarajiwa kuanza Mwezi wa Julai, 2024.
