×

Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo wamekanusha Kutangaza Mgomo – Video

Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam wamekanusha tangazo linalosambaa katika mitandao ya kijamii likieleza kuwa kutakuwa na mgomo kuanzia kesho Juni 23 kutokana na changamoto zao kutosikilizwa na Serikali.

Akizungumza Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo, Hamisi Livembe amesema tangazo hilo halijatoka katika jumuiya hiyo na hawana taarifa juu ya nani aliyehusika kuandika ujumbe huo.

“Hatujafahamu ni nani ameandika kwakweli, lakini taarifa tulizozipata ni kwamba Serikali kupitia TCRA wanafuatilia wao kujua limetoka wapi, kwa sababu kwakweli halikutoka miongoni mwetu,” ameeleza.

Akizungumzia kuhusu kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhusu changamoto za wafanyabiashara, amesema katika bajeti ya mwaka jana zilichukuliwa changamoto tisa kati ya 21, na zilizobakia Serikali iliahidi kuzishughulikia katika bajeti ya mwaka huu, lakini katika bajeti iliyosomwa bungeni hayakutajwa.

Leave a Comment