
Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bw. Leonard Mususa akizungumza na wanahisa wakati wa hafla ya Mkutano Mkuu wa 51 wa mwaka wa Kampuni hiyo ambao ulifanyika jana kwenye kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.Mkutano huo uliangazia utendaji wa kifedha wa TBL PLC, mikakati na nafasi yake katika soko. Kushoto ni Katibu wa Kampuni Bi. Esther Kuja na kulia ni Mjumbe wa Bodi Bw. Phocus J. I. Lasway.
