×

Rais Samia Apongeza Miradi Inayozalishwa na Chuo Kikuu cha SUA (Picha +Video)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuweka jiwe la Msingi la msingi ujenzi wa Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) katika eneo la Kiwanda cha uchakataji tumbaku Mkwawa (MTPL) Mkoani Morogoro tarehe 06 Agosti, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inaunga mkono juhudi zinazofanywa na vyuo vinavyotoa mafunzo ya kilimo kwa kuongeza tija mashambani, hayo yamesemwa leo Agosti 6, 2024 kwenye ziara katika Chuo Kikuu cha Sokoine Morogoro.

Aidha Rais Samia ameipongeza miradi mbalimbali inayozalishwa na Chuo hiko ikiwa pamoja na kutoa mafunzo kwa vikundi na kuwapatia ajira, pia amevitaka Vyuo vingine viige kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine.

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua jengo Mtambuka la Mafunzo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwenye Kampasi ya Edward Moringe, Mkoani Morogoro tarehe 06 Agosti, 2024.
Rais Samia akiteta jambo na Mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha uchakataji tumbaku Mkwawa (MTPL) na Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) Ahmed Huwel wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) Mkoani Morogoro tarehe 06 Agosti, 2024.
Rais  Samia Suluhu Hassan aweka jiwe la msingi ujenzi wa Kiwanda cha Sigara cha Serengeti (SCC) katika eneo la Kiwanda cha uchakataji tumbaku Mkwawa (MTPL).

Leave a Comment