×

Waendesha Baiskeli Wamuaga Mama Maria Nyerere Wakianza Safari ya Butiama Kesho

Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere (katikati) akizungumza kwenye hafla ya msafara wa waendesha baiskeli wa Twende Butiama 2024 walipokwenda kumuaga. Kushoto ni mwanasiasa mkongwe wa hapa nchini, Getruda Mongela na kulia ni Afisa wa Vodacom ambao ndiyo wadhamini wa safari hiyo. 

Waendesha baskeli zaidi ya 10 kesho asubuhi wakiwa wanatarajia kuanza safari ya kuelekea Butiama katika kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere leo wamemtembelea na kumuaga mjane wake, Mama Maria Nyerere.

Kiongozi wa msafara huo, Gabriel Landa akizungumza na baadhi ya washiriki wa safari hiyo.

Safari hiyo iliyodhaminiwa na Kampuni ya Simu ya Vodacom inatarajiwa kuanza kesho asubuhi kwenye viwanja vya Posta jijini Dar huku waendesha baiskeli kutoka mataifa kadhaa ikiwemo Kenya, Kongo DRC na Burundi na nao wanashiriki mbio hizo.

Mmoja wa washiriki wa safari hiyo, akimuaga Mama Maria Nyerere anayepunga mkono akiwa amekaa.

Akizungumza nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, Dar kiongozi wa msafara huo, Gabriel Landa amesema wanatarajia kuanza msafara huo kesho majira ya alfajili ambapo wanatarajia kuwasili Butiama Oktoba 13 na kuungana na Watanzania wengine katika kumbikizi ya miaka 25 tangu kifo cha Hayati Baba wa Taifa.  HABARI/PICHA RICHARD BUKOS NA NEEMA ADRIAN /GPL  

Leave a Comment