
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Mafia amepokea Kibali cha Ajira Mpya kwa Ikama ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na. FA.97/288/01/09 cha tarehe 25 Juni, 2024 kwa upande wa nafasi za Msaidizi wa
Kumbukumbu Daraja la II na Kibali cha Ajira Mbadala chenye Kumb.
Na.FA.228/613/01/D/065 cha tarehe 09 Julai,2024 kwa upande wa nafasi ya Mtendaji wa Kijiji Daraja la III. Hivyo Watanzania wote wenye sifa wanatangaziwa kutuma maombi ya kazi kwa nafasi zifuatazo:-
