×

Samia Kalamu Awards: Waandishi Wapongezwa kwa Kuelimisha Umma Kuhusu Nishati Safi (Picha +Video)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Viongozi, Wadau wa habari pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya utoaji wa Tuzo za Samia Kalamu Awards2025 kwa Waandishi wa Habari katika ukumbi wa The Super Dome Masaki Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Mei, 2025.

Rais Samia Suluhu Hassan amewapongeza waandaaji wa Tuzo za Samia Kalamu Awards kutokana na tuzo hizo kuangazia pia eneo la Nishati Safi ambalo ni ajenda ya Tanzania Kimataifa na kusema kuwa amefurahi sana kuona waandishi wa Habari wanaandika kuhusiana na sekta hiyo.

Rais Samia kwenye picha ya pamoja na Mama Getrud Mongela.

Akizungumza mara baada ya kutoa tuzo hizo, Rais Samia amesema, suala la Nishati safi ni ajenda ya Tanzania na kilichofanyika kwa wanahabari katika kukuza ajenda hiyo ni jambo ambalo linaonesha uzalendo mkubwa.

Amesema, ajenda ya Nishati Safi itasaidia utunzaji wa mazingina kwani takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya hekari laki 4 za misitu zinakatwa ili kupata nishati kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Rais Samia akitoa Tuzo kwa Mwandishi wa Habari Mbobevu Mariam Hamdani.
Rais Samia akitoa Tuzo pamoja na mfano wa hundi ya shilingi milioni 20 kwa Mwandishi wa Habari Mbobevu Ndugu Tido Mhando